RESEARCH AD

RESEARCH AD

CLEARING AND FORWADING

CLEARING AND FORWADING

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

THE GUARDIAN LTD

Saturday, November 16, 2013

MZUMBE GRADUATION

Graduation

Mzumbe University will hold its 12th graduation ceremonies as follows:
  • Main Campus - Friday, 6th December, 2013 starting at 10.00 am.
  • Mbeya Campus College - Friday 13th December, 2013 from 1.00pm.
  • Dar es Salaam Campus College Friday, 20th December, 2013 at Diamond Jubilee Hall in Dar es Salaam starting at 2.00 pm.
Read More >>
Source:mzumbe.ac.tz
NAFASI ZA SKOLASHIPU NCHINI PAKISTAN (MASTERS DEGREE)




Serikali ya Pakistani inatangaza nafasi  za Ufadhili wa Masomo ya Chuo Kikuu katika Ngazi ya MASTERS  kwa mwaka wa masomo 2014.

Waombaji wa nafasi hizo wanatakiwa kuingia katika Mtandao ufuatao ili kupata Fomu za maombi, kuzijaza, kuzi-scan na hatimae kuzituma PAKISTANI kabla ya tarehe 25 Novemba, 2013
.

www.comsats.edu.pk
Ikumbukwe kuwa mwombaji atatakiwa kuchangia sehemu ya gharama ya masomo kama inavyoelekezwa katika matangazo yanayopatikana katika website iliyotajwa hapo juu.
Source:moe.go.tz

Tuesday, November 12, 2013

KOREAN GOVERNMENT SCHOLARSHIP PROGRAM FOR INTERNATIONAL STUDENTS





 
KOREAN GOVERNMENT SCHOLARSHIP PROGRAM FOR INTERNATIONAL STUDENTS FOR UNDERGRADUATE DEGREE TENABLE IN KOREA FOR THE YEAR 2014

Applications are invited from qualified Tanzanians for undergraduate scholarships tenable in Korea for the year 2014.

Wednesday, November 6, 2013

SERIKALI YAWEWESEKA NA ''ZIRO'' YAKE
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge Mh. William Lukuvi

KATIKA kile kinachoonekana kuwa ni kuweweseka kwa serikali katika sakata la kufuta daraja sifuri katika mitihani ya kidato cha nne na sita, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, jana alilazimika kumkana Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome.
Lukuvi alisema taarifa aliyoitoa Mchome wiki iliyopita kuwa serikali imefuta daraja sifuri kwa kidato cha nne na sita haikuwa ya serikali, bali ile iliyotolewa juzi na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo, kuwa haijafutwa ndiyo sahihi.
Lukuvi alitoa kauli hiyo mara baada ya Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (CHADEMA), kuomba mwongozo wa Spika akitaka kujua hatua watakazochukuliwa mawaziri wa wizara hiyo kwa kulidanganya Bunge na umma.

Tuesday, November 5, 2013

Maaskofu wapinga alama mpya za mitihani

Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (Tec), ‘limeuponda’ uamuzi wa serikali wa kushusha viwango vya ufaulu kwa mitihani ya kidato cha nne na sita, likisisitiza kuwa hatua hiyo ni upungufu na ishara ya kuporomoka kwa siasa na ni kipimo kitakachoitumbukiza elimu shimoni.
Kauli hiyo ya Tec, imekuja wakati serikali imetangaza rasmi kuanza kutumika kwa mfumo mpya wa usahihishaji wa mitihani na upangaji wa viwango vya madaraja ya ufaulu, uamuzi ambao hata hivyo, umelifuta daraja sifuri, kuanzia mwakani.

Rais wa baraza hilo, Askofu Tarcius Ngalalekumtwa, akizungumza katika mahafali ya sita ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu, Mwenge (Mwuce), kilichopo Wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, alisema kitendo hicho kinaishangaza dunia kutokana na wenye dhamana kubadili maneno katika kushughulikia elimu na kwamba hali siyo nzuri katika sekta hiyo kwa sababu 'hatutaki kutafuta ni wapi tulipojikwaa na kutufikisha hapo tulipo.'

Mabadiliko hayo na utaratibu wa kuimarisha mfumo huo wa ufaulu, utaanza kutumika katika kupanga matokeo ya kidato cha nne na sita kwa
mwaka 2013/2014, wakati umma ukiwa bado unahoji kilicho nyuma ya pazia juu ya matokeo ya aibu ya mwaka jana ya kidato cha nne baada ya asilimia 60 ya watahiniwa wote kupata daraja sifuri.
LOWASSA: MPANGO WA MATOKEO MAKUBWA SASA HAUNA MENO


Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa amesema ana shaka kama Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Result Now), utafanikiwa kutokana na Kitengo cha Utekelezaji, Ufuatiliaji na Tathmini ya Miradi ya Maendeleo kilicho chini ya Ofisi ya Rais (PDB) kukosa meno.

Akichangia mjadala wa hoja ya Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2014/2015, Lowassa alisema tatizo kubwa linaloikabili nchi ni viongozi kushindwa kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo.

“Tatizo la nchi hii mnazungumza mambo mengi lakini hakuna utekelezaji,” alisema Lowassa wakati akichangia mjadala huo uliowasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira, wiki iliyopita.
Chanzo: Mwananchi

Saturday, November 2, 2013

WASOMI WADAI MABADILIKO MITIHANI YA SEKONDARI NI SIASA TU



Siku moja baada ya Serikali kutangaza kupunguza viwango vya ufaulu kwa mtihani ya kidato cha nne na sita, baadhi ya wasomi na wadau wa elimu wameponda uamuzi huo na kusema una malengo ya kisiasa.

Baadhi ya wadau hao wakizungumza na gazeti hili jana, walisema Tanzania imeweka rekodi kwa nchi za Afrika kwa kuwa na kiwango kidogo sana cha ufaulu cha alama F kuanzia 0 mpaka 19.

Walisema, Serikali imechukua uamuzi huo kisiasa ili kuhakikisha kuwa, wanatimiza lengo la Mpango wa Maendeleo Makubwa Sasa (BRN), ambalo ni kuhakikisha matokeo ya ufaulu kwa Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka huu yanafikia asilimia 60 kutoka 33 ya mwaka jana.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Herme Mosha alisema kuwa kilichofanywa na Serikali ni kupanua wigo wa watu kufaulu.

WARIOBA ATAKA ELIMU CHUO KIKUU IBORESHWE


Rais wa Umoja wa waliokuwa wanafunzi wa Chuo Kkuu cha Dar es Salaam, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amewataka wahitimu wa chuo hicho kuungana kukisaidia kuboresha miundombinu na ubora wa elimu.

Jaji Warioba, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba alisema hayo juzi wakati umoja huo walipokutana kujadiliana jinsi ya kuboresha chuo hicho kwa kutoa michango yao pasipo kusubiri jukumu hilo kufanywa na Serikali.

Warioba alisema hali ya chuo ni ngumu kutokana na kuchakaa kwa miundombinu mbalimbali, uhaba wa walimu na vitendea kazi, jambo ambalo aliwataka kuunganisha nguvu kusaidia mabadiliko.

SERIKALI KUSOMESHA BURE WANAFUNZI WA UDAKTARI 

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ipo katika mchakato wa kuhakisha wanafunzi wote wanaochukua masomo ya Shahada ya Kwanza ya Udaktari kwenye vyuo binafsi na mashirika ya kidini wanagharamiwa bure na Serikali. Hayo yalibainishwa jana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi,alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Rita Mlaki(CCM).

Mbunge huyo alisema Jiji la Dar es Salaam lina takriban watu milioni tano na wote hukimbilia kupata huduma katika Hospitali za Amana, Mwananyamala na Temeke.
Alihoji ni lini Serikali itawalipia ada wanafunzi wote wanaochukua shahada ya udaktari hata wale wanaosoma katika vyuo binafsi ikiwamo Chuo cha IMTU ili kuongeza idadi ya madaktari.


HR INFORMATION SYSTEM COURSE
MZUMBE UNIVERSITY
DIRECTORATE OF EXTERNAL LINKAGES AND COMMUNITY ENGAGEMENT (DELCE)
SHORT COURSE ANNOUNCEMENT

COURSE TITLE: EFFECTIVE MANAGEMENT OF HUMAN RESOURCE USING COMPUTERIZED HUMAN RESOURCE MANAGEMENT INFORMATION SYSTEM
EMPLOYMENT OPPORTUNITIES

MZUMBE UNIVERSITY

VACANCIES
The Mzumbe University invites applications from suitably qualified and competent applicants to fill the following vacant posts...

Friday, October 25, 2013

NOTICE TO LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION IN THEIR APPLICATION FORMS 

During the exercise of processing 2013/2014 loan application forms, the Higher Education Students’ Loans Board came across 6,364 loan applications which were missing some vital information for further loans processing. Six problems were identified as follows:
·        No Applicant’s Signature,
·        No Birth Certificate,
·        No Guarantor’s Photo,
·        No Guarantor’s Signature
·        Not Signed by Local Authority
·        Not Signed by the Magistrate
For that reason, the Board informed concerned Loan applicants that such incomplete applications would have not been considered until the missing information was provided.  However, until the deadline only 3,151 loan applicants had corrected their forms in time.
The Board is hereby once again giving a second chance to the 1,107 first year students loan applicants who have been admitted to priority programmes in various Higher Learning Institutions but did not correct their forms in the earlier provided time (from 16th August to 30th August) to do so within the next 14 days from 24th October to 6th November 2013. These are students who are admitted into the following  Priority programmes:



MADA ZITAKAZOFUNDISHWA NA KUTAHINIWA MWAKA WA KWANZA WA MASOMO KWA WANACHUO WA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI NA STASHAHADA KUANZIA MWAKA 2013/2014

Ili kutekeleza Waraka wa Elimu namba 3 wa mwaka 2013, Wizara imeainisha mada zitakazofundishwa na kutahiniwa mwaka wa kwanza wa masomo kwa wanachuo wa mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti na stashahada. Kila mkuu wa Chuo, Wakufunzi pamoja na Wanachuo wote wa mwaka wa kwanza wa kila Chuo wanaelekezwa kuzingatia maelekezo hayo ili kufanikisha utekelezaji wa Waraka husika.

icon Mada zitakazofundishwa na kutahiniwa mwaka wa kwanza wa masomo ngazi ya cheti na stashahada (107.03 kB)

Monday, October 21, 2013

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI NYONGEZA MWAKA 2013/2014

 MAELEKEZO MUHIMU:

Wanafunzi waliochaguliwa Orodha ya nyongeza kujiunga na Mafunzo ya Ualimu mwaka wa masomo 2013/2014 wanatakiwa kuripoti katika Vyuo walivyopangiwa kuanzia Jumapili tarehe 22/09/2013 hadi 29/09/2013.
Fomu ya maelekezo (joining instruction) zinapatikana kwenye tovuti hii kwa kubofya hapo chini.
Wanafunzi wanatakiwa kufika Vyuoni wakiwa na mahitaji yafuatayo:

 
1. Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani la Tanzania kidato cha NNE;
2. Ada ya muhula wa kwanza sh. 100,000/= au ya mwaka sh. 200,000/=;
3. Sare ya Chuo kulingana na maelekezo ya Chuo husika; na
4. Fedha za tahadhari chuoni na matumizi binafsi.

 
Mkuu wa Chuo anatakiwa kuhakikisha wanafunzi wanaosajiliwa Chuoni ni wale waliopo kwenye orodha hii tu na SI vinginevyo.
Usajili wa kujiunga na Vyuo utafungwa tarehe 29/09/2013 saa 12.00 jioni


GRADE A 2013 Nyongeza
WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA NYONGEZA MWAKA 2013/2014
MAELEKEZO MUHIMU:
 
Wanafunzi waliochaguliwa Orodha ya nyongeza kujiunga na Mafunzo ya Ualimu mwaka wa masomo 2013/2014 wanatakiwa kuripoti katika Vyuo walivyopangiwa kuanzia Jumapili tarehe 22/09/2013 hadi 29/09/2013.
Fomu ya maelekezo (joining instruction) zinapatikana kwenye tovuti hii kwa kubofya hapo chini.
Wanafunzi wanatakiwa kufika Vyuoni wakiwa na mahitaji yafuatayo:

1. Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani la Tanzania kidato cha NNE na cha SITA;
2. Ada ya muhula wa kwanza sh. 100,000/= au ya mwaka sh. 200,000/=;
3. Sare ya Chuo kulingana na maelekezo ya Chuo husika; na
4. Fedha za tahadhari chuoni na matumizi binafsi.

Mkuu wa Chuo anatakiwa kuhakikisha wanafunzi wanaosajiliwa Chuoni ni wale waliopo kwenye orodha hii tu na SI vinginevyo.
Usajili wa kujiunga na Vyuo utafungwa tarehe 29/09/2013 saa 12.00 jioni

icon DIPLOMA-ALPHABETI 2013 Nyongeza (105.93 kB)

| Print |
WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUPATA SKOLASHIPU KWA MPANGO WA KUBADILISHANA WANAFUNZI KATI YA SERIKALI YA TANZANIA NA YA MSUMBIJI MWAKA 2014

Wanafunzi 51 wa Kitanzania wamechaguliwa kujiunga na masomo mbalimbali nchini Msumbiji katika ngazi ya Shahada ya Kwanza kupitia Mpango wa Kubadilishana Wanafunzi kati ya Serikali ya Tanzania na ya Msumbiji (Tanzania – Mozambique Students Exchange Programme – TAMOSE). Masomo yanatarajiwa kuanza juma la Kwanza la Januari, 2014.

Wanafunzi hao ambao orodha yao na masomo watakayosoma vimeambatishwa, wanatakiwa kufika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Idara ya Elimu ya Juu, Chumba Namba 28 kwa ajili ya maelekezo na maandalizi ya safari.

Wanafunzi hao wafike Wizarani kuanzia tarehe 30 Septemba hadi 14 Oktoba 2013 kuanzia Saa 3.00  asubuhi hadi saa 9:30 mchana katika siku za kazi.

Wanafunzi wanashauriwa kufika na nyaraka za kuombea pasi ya kusafiria nje ya nchi – passport (kwa wale ambao hawana). Nyaraka hizo ni pamoja na Cheti cha Kuzaliwa, Picha 5 za passport size zenye rangi ya buluu ya bahari pamoja na gharama za kuombea hati ya kusafiria nje ya nchi Wizara ya Mambo ya Ndani. Kwa wenye passport wanatakiwa kuja nazo.

icon List of Selected Students for Mozambique Scholarships 2014 (38.78 kB)


WAHITIMU WA KIDATO CHA SITA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO MAALUM YA UALIMU (BRIDGING COURSE) MWAKA 2013/2014


MAELEKEZO MUHIMU
Wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na Mafunzo haya wanatakiwa kuripoti Chuo cha Ualimu Morogoro kuanzia tarehe 18/10/2013 hadi 20/10/2013.

Wanafunzi wanatakiwa kufika chuoni wakiwa na mahitaji yafuatayo:
  1. Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani la Tanzania vya Kidato cha NNE na SITA;
  2. Ada ya muhula wa kwanza sh. 100,000/= ;
  3. Sare ya Chuo (Suruali/sketi: koti na tai nyeusi; shati ya mikono mirefu ya rangi ya bluu bahari); na
  4. Fedha za tahadhari chuoni na matumizi binafsi.
Usajili wa waliochaguliwa kujiunga na Mafunzo utafungwa terehe 20/10/2013 saa 12.00 jioni.


icon WAHITIMU WA KIDATO CHA SITA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO MAALUM YA UALIMU (2013/2014) (109.92


MADA ZITAKAZOFUNDISHWA NA KUTAHINIWA MWAKA WA KWANZA WA MASOMO KWA WANACHUO WA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI NA STASHAHADA KUANZIA MWAKA 2013/2014

Ili kutekeleza Waraka wa Elimu namba 3 wa mwaka 2013, Wizara imeainisha mada zitakazofundishwa na kutahiniwa mwaka wa kwanza wa masomo kwa wanachuo wa mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti na stashahada. Kila mkuu wa Chuo, Wakufunzi pamoja na Wanachuo wote wa mwaka wa kwanza wa kila Chuo wanaelekezwa kuzingatia maelekezo hayo ili kufanikisha utekelezaji wa Waraka husika.

icon Mada zitakazofundishwa na kutahiniwa mwaka wa kwanza wa masomo ngazi ya cheti na stashahada (107.03 kB)
NOTICE TO SUCCESSFUL LOAN APPLICANTS FOR 2013/2014 ACADEMIC YEAR  
The Higher Education Students’ Loans Board is hereby announcing names of successful first time loan applicants for 2013/2014 Academic Year who applied and were eligible for student loans.
The list includes the Institution to which the student is admitted to and the amounts of loans allocated to a particular student in all or part of the loanable items as per Guidelines and Criteria for Issuance of Loans and Grants for 2013/2014 Academic Year.
Loan applicants can access their loan status by keying in their Form Four Index Numbers to view the results.
Loan applicants are reminded that the loan money will be sent to their respective institutions where they will be required to sign to acknowledge receipt of the loans, after registration processes.
Issued by:
The Executive Director
Higher Education Students’ Loans Board
P. O. Box 76068