RESEARCH AD

RESEARCH AD

CLEARING AND FORWADING

CLEARING AND FORWADING

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

THE GUARDIAN LTD

Saturday, November 2, 2013

WASOMI WADAI MABADILIKO MITIHANI YA SEKONDARI NI SIASA TU



Siku moja baada ya Serikali kutangaza kupunguza viwango vya ufaulu kwa mtihani ya kidato cha nne na sita, baadhi ya wasomi na wadau wa elimu wameponda uamuzi huo na kusema una malengo ya kisiasa.

Baadhi ya wadau hao wakizungumza na gazeti hili jana, walisema Tanzania imeweka rekodi kwa nchi za Afrika kwa kuwa na kiwango kidogo sana cha ufaulu cha alama F kuanzia 0 mpaka 19.

Walisema, Serikali imechukua uamuzi huo kisiasa ili kuhakikisha kuwa, wanatimiza lengo la Mpango wa Maendeleo Makubwa Sasa (BRN), ambalo ni kuhakikisha matokeo ya ufaulu kwa Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka huu yanafikia asilimia 60 kutoka 33 ya mwaka jana.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Herme Mosha alisema kuwa kilichofanywa na Serikali ni kupanua wigo wa watu kufaulu.

WARIOBA ATAKA ELIMU CHUO KIKUU IBORESHWE


Rais wa Umoja wa waliokuwa wanafunzi wa Chuo Kkuu cha Dar es Salaam, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amewataka wahitimu wa chuo hicho kuungana kukisaidia kuboresha miundombinu na ubora wa elimu.

Jaji Warioba, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba alisema hayo juzi wakati umoja huo walipokutana kujadiliana jinsi ya kuboresha chuo hicho kwa kutoa michango yao pasipo kusubiri jukumu hilo kufanywa na Serikali.

Warioba alisema hali ya chuo ni ngumu kutokana na kuchakaa kwa miundombinu mbalimbali, uhaba wa walimu na vitendea kazi, jambo ambalo aliwataka kuunganisha nguvu kusaidia mabadiliko.

SERIKALI KUSOMESHA BURE WANAFUNZI WA UDAKTARI 

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ipo katika mchakato wa kuhakisha wanafunzi wote wanaochukua masomo ya Shahada ya Kwanza ya Udaktari kwenye vyuo binafsi na mashirika ya kidini wanagharamiwa bure na Serikali. Hayo yalibainishwa jana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi,alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Rita Mlaki(CCM).

Mbunge huyo alisema Jiji la Dar es Salaam lina takriban watu milioni tano na wote hukimbilia kupata huduma katika Hospitali za Amana, Mwananyamala na Temeke.
Alihoji ni lini Serikali itawalipia ada wanafunzi wote wanaochukua shahada ya udaktari hata wale wanaosoma katika vyuo binafsi ikiwamo Chuo cha IMTU ili kuongeza idadi ya madaktari.


HR INFORMATION SYSTEM COURSE
MZUMBE UNIVERSITY
DIRECTORATE OF EXTERNAL LINKAGES AND COMMUNITY ENGAGEMENT (DELCE)
SHORT COURSE ANNOUNCEMENT

COURSE TITLE: EFFECTIVE MANAGEMENT OF HUMAN RESOURCE USING COMPUTERIZED HUMAN RESOURCE MANAGEMENT INFORMATION SYSTEM
EMPLOYMENT OPPORTUNITIES

MZUMBE UNIVERSITY

VACANCIES
The Mzumbe University invites applications from suitably qualified and competent applicants to fill the following vacant posts...