RESEARCH AD

RESEARCH AD

CLEARING AND FORWADING

CLEARING AND FORWADING

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

THE GUARDIAN LTD

Tuesday, November 5, 2013

Maaskofu wapinga alama mpya za mitihani

Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (Tec), ‘limeuponda’ uamuzi wa serikali wa kushusha viwango vya ufaulu kwa mitihani ya kidato cha nne na sita, likisisitiza kuwa hatua hiyo ni upungufu na ishara ya kuporomoka kwa siasa na ni kipimo kitakachoitumbukiza elimu shimoni.
Kauli hiyo ya Tec, imekuja wakati serikali imetangaza rasmi kuanza kutumika kwa mfumo mpya wa usahihishaji wa mitihani na upangaji wa viwango vya madaraja ya ufaulu, uamuzi ambao hata hivyo, umelifuta daraja sifuri, kuanzia mwakani.

Rais wa baraza hilo, Askofu Tarcius Ngalalekumtwa, akizungumza katika mahafali ya sita ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu, Mwenge (Mwuce), kilichopo Wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, alisema kitendo hicho kinaishangaza dunia kutokana na wenye dhamana kubadili maneno katika kushughulikia elimu na kwamba hali siyo nzuri katika sekta hiyo kwa sababu 'hatutaki kutafuta ni wapi tulipojikwaa na kutufikisha hapo tulipo.'

Mabadiliko hayo na utaratibu wa kuimarisha mfumo huo wa ufaulu, utaanza kutumika katika kupanga matokeo ya kidato cha nne na sita kwa
mwaka 2013/2014, wakati umma ukiwa bado unahoji kilicho nyuma ya pazia juu ya matokeo ya aibu ya mwaka jana ya kidato cha nne baada ya asilimia 60 ya watahiniwa wote kupata daraja sifuri.
LOWASSA: MPANGO WA MATOKEO MAKUBWA SASA HAUNA MENO


Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa amesema ana shaka kama Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Result Now), utafanikiwa kutokana na Kitengo cha Utekelezaji, Ufuatiliaji na Tathmini ya Miradi ya Maendeleo kilicho chini ya Ofisi ya Rais (PDB) kukosa meno.

Akichangia mjadala wa hoja ya Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2014/2015, Lowassa alisema tatizo kubwa linaloikabili nchi ni viongozi kushindwa kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo.

“Tatizo la nchi hii mnazungumza mambo mengi lakini hakuna utekelezaji,” alisema Lowassa wakati akichangia mjadala huo uliowasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira, wiki iliyopita.
Chanzo: Mwananchi